28 Malaika akamwendea, akamwambia, "Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe."
29 Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?
30 Malaika akamwambia, "Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.
31 Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.